Mkutano wa 39 wa Umoja wa Afrika wafunguliwa katikati ya mgogoro unaoongezeka
Mkutano wa 39 wa Umoja wa Afrika unafunguliwa leo Jumamosi asubuhi, Februari 14, huko Addis Ababa, Ethiopia. Wakuu wa nchi na serikali zaidi ya hamsini wanashiriki. Wakati wa sherehe ya ufunguzi, Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika, Mahmoud Ali Youssouf, Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed, Mwenyekiti wa AU anayeondoka, Joรฃo Lourenรงo wa Angola, na mrithi wake, rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye, watahutubia hadhara kuu ya Umoja wa Afrika.