RFI Kiswahili's Avatar

RFI Kiswahili

@sw.rfi.fr

๐ŸŒ Idhaa ya kiswahili ya @RFI.fr (Radio France Internationale) ipo kwa kukuhabarisha habari za kimataifa ๐Ÿ’ป rfi.fr/sw/ ๐ŸŽง rfi.my/mubashara ๐• rfi.my/Xsw ๐Ÿ“ท rfi.my/IGsw ๐Ÿ—จ๏ธ rfi.my/WAsw

47 Followers  |  6 Following  |  4,344 Posts  |  Joined: 03.01.2025  |  1.6361

Latest posts by sw.rfi.fr on Bluesky

Preview
Korea Kaskazini: Kim Jong-un azindua nyumba za familia za wanajeshi waliouawa Ukraine Korea Kaskazini imetuma maelfu ya Wanajeshi kupigana kusaidia Moscow katika mashambulizi yake nchini Ukraine, yaliozinduliwa karibu miaka minne iliyopita, kulingana na mashirika ya ujasusi ya Korea Kusini na nchi za Magharibi. Seoul inasema angalau wanajshi 2,000 wa Korea Kaskazini waliuawa.
16.02.2026 13:36 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Iran yaanza luteka ya kijeshi katika Mlango-Bahari wa Hormuz katikati ya mazungumzo na Marekani Kikosi cha walinzi wa mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), jeshi la kiitikadi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kileanza mazoezi ya kijeshi katika Mlango-Bahari wa kimkakati wa Hormuz leo Jumatatu, Februari 16, kulingana na televisheni ya serikali ya Iran, usiku wa kuamkia mazungumzo ya nyuklia na Marekani huko Geneva.
16.02.2026 12:56 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Mkutano wa kimataifa kuhusu Akili Bandia wafunguliwa India katikati ya wasiwasi unaoongezeka Mkutano wa kimataifa kuhusu Akili Bandia (AI) umefunguliwa leo Jumatatu jijini New Delhi kujadili athari za mapinduzi yanayokuja, kuanzia ajira hadi ulinzi wa watoto, lakini washiriki wana shaka kwamba utatoa hatua madhubuti.
16.02.2026 12:29 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Ujerumani inaona juhudi za Ufaransa katika suala la matumizi ya ulinzi 'hazitoshi' Ujerumani inaona juhudi za Ufaransa katika suala la ulinzi ย "hazitoshi." Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Johann Wadephul ameitaka Ufaransa "kuweka akiba," hasa "katika nyanja ya kijamii," ili "kuwa na uhuru unaohitajika kufikia lengo kuu la uwezo wa ulinzi wa Ulaya." Lengo: 5% ya Pato la Taifa lililotolewa kwa usalama ifikapo mwaka 2035, hatua iliyosukumwa na Donald Trump ndani ya NATO.
16.02.2026 12:15 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
DRC: Marufuku jela ya Makala kupokea wafungwa wapya Waziri wa nchi anayehusika na sheria nchiniย DRC Guillaume Ngefa, amepigaย marufuku kwaย muda uandikishaji wowote mpya wa wafungwa katika gerezaย la Makala jijiniย Kinshasa.
16.02.2026 08:53 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
China yaahidi msaada mpya wa kibinadamu kwa Ukraine: Hatua ya kimkakati China inaahidi msaada mpya wa kibinadamu kwa Ukraine. Beijing inazungumzia haswa wakati diplomasia kuhusu vita ikiwa katika hali tete zaidi. China imetoa msaada wa dharura wa kibinadamu (chakula, dawa) kwa Ukraine, kwa kushirikiana na Shirika la Msalaba Mwekundu.
16.02.2026 07:33 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Ethiopia: Mamlaka ya shirikisho yalaani makubaliano kati ya makundi ya waasi ya Amhara na Tigray Nchini Ethiopia, wakati mvutano huko Tigray ukiongezeka, serikali ya shirikisho inapoteza nguvu katika eneo la Amhara. Katika vita na serikali kwa miaka mitatu, waasi katika eneo la Amhara, pia wanajulikana kama Fano, wanapata tena nguvu na kudhibiti baadhi ya maeneo. Miji muhimu imetekwa tena, ikiwa ni pamoja na Debre Tabor, yapata kilomita 100 kutoka mji mkuu wa eneo hilo. Ndege zisizo na rubani zilishambulia mji huo mara kadhaa wiki iliyopita.
16.02.2026 06:52 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Wapiganaji wa Kiafrika kwa ajili ya Urusi: Mtandao wa uajiri unailenga hasa Cameroon Cameroon ni mojawapo ya nchi kuu za asili ya wapiganaji wa Kiafrika wanaohudumu katika jeshi la Urusi nchini Ukraine, kulingana na matokeo ya uchunguzi uliofanywa na kundi la All Eyes on Wagner.
16.02.2026 06:25 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Ghana yataka UM kutambua biashara ya utumwa Afrika kama 'uhalifu mbaya zaidi dhidi ya binadamu' Ghana itawasilisha azimio kwa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa mwezi Machi ili kutaja biashara ya utumwa barani Afrika kama "uhalifu mbaya zaidi dhidi ya binadamu," Rais wa Ghana John Dramani Mahama ametangaza siku ya Jumapili.
16.02.2026 05:58 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Mkutano wa Umoja wa Afrika watamatika: 'Hakuna uvumilivu kwa mapinduzi kinyume cha Katiba' Mkutano wa 39 wa Umoja wa Afrika sasa umekamilika. Kwa siku mbili, wakuu wa nchi na serikali, wanachama wa Umoja wa Afrika, walijadili migogoro mikubwa inayoathiri bara hilo. Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye, ambaye alichukua nafasi ya uenyekiti wa kupokezana wa AU katika mkutano huu, na Mwenyekiti wa Tume, Rais wa Djibouti Mahmoud Ali Youssouf, waliwasilisha hitimisho kuu katika mkutano wa mwisho na waandishi wa habari siku ya Jumapili, Februari 15.
16.02.2026 05:32 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Reza Pahlavi atoa wito wa kuingilia kati kijeshi 'haraka' nchini Iran Mtoto wa Shah aliyeondolewa madarakani, Reza Pahlavi, ametoa wito tena kwa Donald Trump kwa kuingilia kati kijeshi "haraka" nchini Iran na akarudia pendekezo lake la kuhakikisha "mpito" wa kisiasa nchini Iran, akizungumza kwenye Fox News siku ya Jumapili, Februari 15.
16.02.2026 05:05 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Kenyaย : Mpasuko waendelea kushuhudiwa katika chama cha ODM Nchini Kenya, mpasuko wa kisiasa ndani ya chama cha siasa cha ODM umeendelea ambapo mwishoni mwa wiki iliyopita, pande mbili zinazovutana kuhusu kumuunga mkono rais William Ruto, ziliandaa mikutano ya hadhara.
16.02.2026 05:05 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Watu wasiopungua ishirini wamefariki baada ya shambulio kubwa kaskazini mwa Burkina Faso Mji wa Titao, ambao hapo awali haujakumbwa na mashambulizi ya kigaidi, ulivamiwa na kundi la washambuliaji siku ya Jumamosi, Februari 14, 2026. Walishambulia na kupora kambi ya kijeshi. Mashahidi wanaripoti kwamba waasi walichoma moto soko la mji huo na kuharibu miundombinu ya mawasiliano ya simu. Msemaji wa vikosi vya jeshi, Luteni Kanali Abdoul Aziz Ouedraogo, alithibitisha shambulio hilo siku ya Jumapili jioni, Februari 15, kwenye televisheni ya kitaifa.
16.02.2026 04:51 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Mazungumzo kati ya Iran na Marekani: Netanyahu yaweka masharti ya makubaliano Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ametoa wito siku ya Jumapili kwa "kuvunjwa" kwa uwezo wa urutubishaji wa uranium wa Iran, wakati wa hotuba mbele ya Mkutano wa viongozi wa mashirika ya Kiyahudi ya Marekani.
16.02.2026 04:51 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Nyuklia, mafuta, gesi, madini... Kile Iran inapendekeza ili kurahisisha makubaliano na Marekani Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameondoka Tehran Jumapili, Februari 15, kwenda Geneva kwa ajili ya duru ya pili ya mazungumzo na Marekani, yanayosimamiwa na Oman, ili kuzuia mashambulizi ya Marekani. Iran inatafuta kuhitimisha makubaliano ya nyuklia na Marekani ambayo yangeleta faida za kiuchumi kwa pande zote mbili, mwanadiplomasia wa Iran alisema siku ya Jumapili.
16.02.2026 04:37 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Kambi ya kijeshi yashambuliwa na kuporwa nchini Mali Nchini BurkinaFaso, mji wa Titao, ambao hapo awali uliokolewa kutokana na mashambulio ya kigaidi, ulivamiwa na kundi la washambuliaji siku ya Jumamosi, Februari 14, 2026. Walishambulia na kupora kambi ya kijeshi.
16.02.2026 04:37 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Mapigano FIzi, DRC: 'Bado tunashambuliwa kwa mabomu na ndege zisizo na rubani za serikali' Wakati usitishaji mapigano ukitarajiwa kuanza siku ya Jumatano, Februari 18, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), mapigano makali yanayoambatana na mashambulizi ya mabomu yanaendelea katika nyanda za juu za Minembwe, katika eneo la Fizi katika mkoa wa Kivu Kusini, kati ya wapiganaji wa Twirwanehoโ€”wanaoshirikiana na AFC/M23โ€”na jeshi la Kongo, linaloungwa mkono na jeshi la Burundi na wanamgambo wa Wazalendo.
15.02.2026 14:40 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
DRC: Gereza Kuu la Makala jijini Kinshasa lakumbwa na kipindupindu Ugonjwa wa kipindupindu unaenea ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na kufikia gereza kubwa zaidi nchini humo la Makala, jijini Kinshasa. Vifo vimeripotiwa katika gereza hilo. Wagonjwa kadhaa wamethibitishwa miongoni mwa wafungwa. Mamlaka ya mahakama imetangaza hatua za dharura kujaribu kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huo.
15.02.2026 10:11 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
China kufutia ushuru karibu nchi zote za Afrika mwezi Mei China itafuta ushuru kwa nchi zote za Afrika, isipokuwa Eswatini, kuanzia Mei 1, Rais wa China Xi Jinping ametangaza siku ya Jumamosi, kulingana na vyombo vya habari vya serikali.
15.02.2026 09:57 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Mafuta: Libya yafungua milango yake kwa makampuni ya kigeni Kwa mara ya kwanza katika miaka 17, Libya ilitoa vitalu vya mafuta kwa makampuni ya kigeni Jumatano, Februari 11, 2026. Kampuni ya Marekani Chevron, kampuni ya Uingereza BP, kampuni ya Italia ENI, na kampuni ya Nigeria Aiteo Group wataweza kuchunguza na kutumia ardhi ya chini ya Libya, kwa ushirikiano na NOC, kampuni ya serikali ya mafuta.
15.02.2026 09:44 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Niger: Jenerali Abdourahamane Tiani azidisha mashambulozi yake ya maneneo kwa Ufaransa Kiongozi wa utawala wa kijeshi wa Niger, Jenerali Abdourahamane Tiani, amehutubia taifa kwa zaidi ya saa tatu katika ujumbe uliofuatwa na mahojiano marefu yaliyorushwa kwenye RTN - redio na televisheni vya serikali - ambapo Jenerali Tiani ameelezea hali ya usalama, uchumi, na kidiplomasia nchini Niger, akiikosoa mara kwa mara "Ufaransa na vibaraka wake wa Afrika Magharibi."
15.02.2026 09:30 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Mwenyekiti wa Kamati ya AU: 'Kuangamizwa' kwa watu wa Palestina 'lazima kukome' Mkutano wa 39 wa kila mwaka wa Umoja wa Afrika (AU) umefunguliwa Jumamosi, Februari 14, huko Addis Ababa, Ethiopia. Katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Tume ya AU, Mahamoud Ali Youssouf, rais wa Djibouti, alitaka kukomeshwa kwa kile alichokielezea kama "kuangamizwa" kwa watu wa Palestina.
15.02.2026 09:17 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
DRC: Wanamgambo wa Erik Prince wapelekwa Uvira kusaidia jeshi katika kulinda mji Erik Prince, mfuasi wa Rais wa Marekani Donald Trump, amewatuma wanamgambo wa kampuni yake binafsi ya kijeshi kusaidia kulinda mji wa Uvira, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), kulingana na vyanzo vilivyohojiwa na shirika la habari la Reuters. Mji huu wa mkoa wa Kivu Kusini ulitekwa kwa muda mfupi na waasi wa M23 mnamo mwezi Desemba 2015.
15.02.2026 07:42 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Mpango wa Mattei: Giorgia Meloni azindua upya mkakati wake wa Afrika Addis Ababa Miaka miwili baada ya uzinduzi wa "Mpango wa Mattei" huko Roma, Giorgia Meloni ametumia fursa ya ziara yake yake kwenda Addis Ababa siku ya Ijumaa, Februari 13, kando ya mkutano wa kilele wa Umoja wa Afrika, ili kuthibitisha tena matarajio ya Italia barani humo. Waziri Mkuu wa Italia alisisitiza ushirikiano "kati ya usawa," huku pia akitangaza kwamba alikuwa akifanya kazi kwenye deni linalohusiana na mishtuko ya hali ya hewa.
15.02.2026 07:28 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Marekani: Mahakama ya Shirikisho inalinda haki za wakimbizi wa Sudan Kusini Jaji wa Shirikisho Patti Saris alizuia uamuzi wa utawala wa Trump siku ya Alhamisi, Februari 12, 2026, wa kukomesha ulinzi wa muda dhidi ya kufukuzwa kwa wakimbizi wa Sudan Kusini. Tangu mwaka 2011, wamekuwa na hadhi hii maalum nchini Marekani, ambayo pia inawahakikishia vibali vya kufanya kazi, lakini utawala wa Trump unatafuta kukomesha hadhi hiyo.
14.02.2026 07:51 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
DRC: Mkuu wa MONUSCO ajadili utaratibu wa ufuatiliaji wa kusitisha mapigano na AFC/M23 Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini DRC, MONUSCO, unaendelea na maandalizi yake ya kuanzishwa kwa utaratibu wa ufuatiliaji wa uwezekano wa kusitisha mapigano ambao unaweza kufuata mipango ya hivi karibuni ya kidiplomasia. Kaimu mkuu wa MONUSCO, Vivian van de Perre, alikuwa Goma kwa saa 48 zilizopita kukutana na pande mbalimbali zinazohusika.
14.02.2026 07:51 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Chad: Mfaransa aliyetoweka katika eneo la Amdjarass apatikana amefariki Mtalii, raia wa Ufaransa, amepatikana amekufa katika oasisi (chemchemi) ya Bachikรฉlรฉ, yapata kilomita 100 kutoka Amdjarass, mji mkuu wa jimbo la Ennedi Mashariki nchini Chad. Mstaafu huyo mwenye umri wa miaka 70, kutoka Dijon, Ufaransa, alitoweka tangu siku ya Jumatano baada ya kuanza safari ya kutembelea oasisi ya Bachikรฉlรฉ akiwa na watalii wengine zaidi ya hamsini waliohudhuria Tamasha la Kimataifa la Tamaduni za Sahara (FICSA).
14.02.2026 07:37 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Uganda: Wabunge watoa wito wa uchunguzi kuhusu uhalifu unaowezekana dhidi ya binadamu Bunge la Ulaya limepitisha azimio kuhusu hali ya baada ya uchaguzi nchini Uganda. Siku ya Alhamisi, Februari 14, 2026, Wabunge wa Umoja wa Ulaya walipiga kura kuunga mkono nakala inayolaani ukandamizaji dhidi ya upinzani, mahirika ya kiraia, na vyombo vya habari kufuatia uchaguzi wa urais wa Januari 15, na kutoa wito wa uchunguzi huru kuhusu madai ya ukiukwaji. Nakala hiyo, iliyopitishwa na idadi kubwa ya wabunge, imeibua hisia chanya kutoka kwa upinzani nchini Uganda.
14.02.2026 07:10 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Mkutano wa 39 wa Umoja wa Afrika wafunguliwa katikati ya mgogoro unaoongezeka Mkutano wa 39 wa Umoja wa Afrika unafunguliwa leo Jumamosi asubuhi, Februari 14, huko Addis Ababa, Ethiopia. Wakuu wa nchi na serikali zaidi ya hamsini wanashiriki. Wakati wa sherehe ya ufunguzi, Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika, Mahmoud Ali Youssouf, Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed, Mwenyekiti wa AU anayeondoka, Joรฃo Lourenรงo wa Angola, na mrithi wake, rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye, watahutubia hadhara kuu ya Umoja wa Afrika.
14.02.2026 06:57 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0
Preview
Michuano ya AFCON haitaahirishwa wasiwasi, atangaza mkuu wa CAF Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) ambayo imekutana jijini Dar es Salaam siku ya Ijumaa hii, Februari 13, imebainisha kwamba michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika la 2027 haitaahirishwa, licha ya wasiwasi unaohusiana na maandalizi ya miundombinu na hali ya kisiasa katika nchi wenyeji. Kamati hiyo pia imejadili matukio yaliyotokea wakati wa fainali iliyopita na kuahidi kuimarisha nidhamu na usuluhishi.
13.02.2026 15:39 โ€” ๐Ÿ‘ 0    ๐Ÿ” 0    ๐Ÿ’ฌ 0    ๐Ÿ“Œ 0

@sw.rfi.fr is following 6 prominent accounts